Home » » TAKUKURU: YAOKOA SHILINGI BILIONI 39 NA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA VITENDO VYA RUSHWA KWA WAHUSIKA

TAKUKURU: YAOKOA SHILINGI BILIONI 39 NA KUCHUKUA HATUA DHIDI YA VITENDO VYA RUSHWA KWA WAHUSIKA

 
Mkurugenzo mkuu wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU nchini EDWRD HOSEA amesema taasisi hiyo imefanikiwa kuokoa zaidi ya shilingi bilioni 39 katika kipindi cha kuanzia mwezi januari hadi Disemba mwaka jana kutokana na kuchukua hatua dhidi ya vitendo vya rushwa katika idara mbalimbali za serikali.
Mkurugenzi mkuu wa takukuru ameeleza hayo wakati akifungua jengo jipya la ofisi za taasisi hiyo katika manispaa ya kigoma ujiji, jengo lililogharimu zaidi ya shilingi bilioni 1.2 ambapo amesema katika kipindi hicho kesi 256 zilifunguliwa na taasisi hiyo na kwamba wamejikita zaidi katika kusimamia maadili, ushirikishwaji wa umma na kuheshimu utawala ambapo ameitaka jamii kuitumia taasisi hiyo kukabiliana na rushwa katika idara mbalimbali na katika uchaguzi ili kupata viongozi bora.
 
Kwa upande wake mkuu wa takukuru mkoa wa kigoma SUZAN RAYMOND na katibu tawala wa mkoa wa kigoma JOHN NDUNGURU wamesema zaidi ya kesi sita ziko zinaendelea katika mahakama mbalimbali mkoani kigoma na kwamba wamejipanga kupambana na vitendo vya rushwa katika kipindi cha uchaguzi mkuu ujao.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Chanzo :ITV Tanzania

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa