Home » » WANANCHI SIMIYU WAENDELEA NA USAJILI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA

WANANCHI SIMIYU WAENDELEA NA USAJILI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Mkoa wa Simiyu ni miongoni mwa mikao 12 ya Tanzania inayoendelea na zeozi la kuwasajili wananchi kwa lengo la kuwapatia Vitambulisho vya Taifa.
Kwa sasa zoezi hilo limeingia kwenye awamu ya pili ya Usajili katika wilaya zote za mkoa huo ambazo ni Bariadi, Meatu, Busega, Maswa na Itilima huku mwitikio wa watu ukiwa mkubwa.
wanaoshiriki kwenye zoezi hilo ni wananchi wote wenye umri wa miaka 18 na kuendelea, wageni na Wakimbizi.

Pichani ni Maafisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) wakiwachukua alama za Kibaiolojia wananchi wa mkoa wa Simiyu Kijiji cha  Mwakiboro wakati zoezi la Usajili likiendelea .
Zoezi la Usajili likiendelea katika Kijiji cha Kilulu wilayani Bariadi 

Wananchi wa Kijiji cha Mwakiboro mkoani Simiyu wakisubiri kupatiwa huduma ya Uandikishwaji Vitambulisho vya Taifa.
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa