Home » » DK.KAMANI AONYA WATAKAO HUJUMU MIRADI

DK.KAMANI AONYA WATAKAO HUJUMU MIRADI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WAZIRI wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Titus Kamani, amewaonya watendaji watakaotafuna fedha za miradi mbalimbali inayotekelezwa Jimbo la Busega mkoani Simiyu.
Dk. Kamani, alitoa onyo hilo juzi wakati akikagua mradi wa maji Kijiji cha Nyangili, Kata ya Igalukilo Busega mkoani Simiyu, ambako pamoja na mambo mengine alikagua miradi mbalimbali inayotekelezwa katika kata hiyo.
Alisema mradi huo umetumia fedha nyingi ambazo si bajeti ya serikali, bali juhudi zake binafsi kama mwakilishi wa wananchi hao, akiwashirikisha wadau mbalimbali wakiwemo marafiki, wahisani pamoja na Benki ya Dunia.
“Nawaomba ndugu zangu muulinde mradi huu na kuhakikisha wananchi wanahudumiwa bila kubaguliwa,” alisema.
Mradi huo wa maji katika Kijiji cha Nyangili, umegharimu sh mil. 300 ikiwa ni fedha kutoka Benki ya Dunia.
Dk. Kamani, aliitaja miradi inayotekelezwa Kata ya Igalukilo kuwa ni pamoja na mradi wa umeme unaopita Kijiji cha Nyangili, Lunala na Mwamagigisi na mradi wa ujenzi wa nyumba za watumishi wa kituo cha afya Igalukilo.
Upande wa ujenzi wa barabara, Dk. Kamani alisema kuwa miradi ya barabara imetengewa sh mil. 300 ambapo barabara ya Mwamjulila na Badugu itatengenezwa na itapitika kwa urahisi kuliko ilivyokuwa awali.
 Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa