Home » » WANANCHI WATAKIWA KULINDA HIFADHI ZA TAIFA

WANANCHI WATAKIWA KULINDA HIFADHI ZA TAIFA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WANANCHI wametakiwa kuzilinda na kuzihifadhi Hifadhi za Taifa, ili ziweze kuwa endelevu kwa sababu zina manufaa mengi kwa jamii.
 Kauli hiyo ya ilitolewwa mjini hapa juzi na Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Titus Kamani, alipokuwa akifungua mradi wa bwawa la maji katika kitongoji cha Mwabayanda, kilichoko kijiji cha Lamadi, wilayani Busega mkoani Simiyu.
 Alisema bwawa hilo lililochimbwa na Shirika la Hifadhi za Taifa (Tanapa), kupitia Hifadhi yaTaifa ya Serengeti, ni mkombozi kwa wananchi hao, kwani litawaondolea kero ya maji iliyodumu kwa muda mrefu.
 Alisema kutokana na faida hiyo ya kupata maji kwa ajili ya matumizi ya binadamu na mifugo, pamoja na miradi mingine,  ni vema sasa wananchi wakazithamini na kuzitunza hifadhi za taifa, ili ziendelee kuwaletea maendeleo zaidi.
 Waziri Kamani ambaye pia ni mbunge wa Busega, aliwataka wananchi kulitunza bwawa hilo, ili liweze kuwa endelevu, sanjari na kuunda kamati ya maji itakayosimamia mradi huo.
 Pia aliwataka wananchi kuacha kunywesha mifugo yao ndani ya bwawa hilo na badala yake wazinyweshe kwenye miundombinu iliyowekwa pembezoni.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa