Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kuanza upya kujitokeza mauaji ya walemavu wa ngozi (Albino)
mkoani Simiyu, kumesababisha wananchi kuomba Serikali kuwawekea ulinzi
mkali walemavu hao ili waishi kwa amani.
Hatua hiyo inatokana na mauaji ya mkazi wa
Kitongoji cha Chalala, Kijiji cha Gasuma, Kata ya Mwaubigi, wilayani
Bariadi, Munghu Lugata (40) kuuawa kikatili kwa kukatwa viungo vyake.
Wananchi waliojitokeza kwenye mazishi ya Lugata
juzi, walisema walemavu wa ngozi wanatakiwa wasiishi peke yao, bali
wakae na watu wengine ili kulinda usalama wa. Mwanamke huyo alikuwa
akiishi na mtoto mdogo.
Dada wa marehemu, Minza Lugata alisema siku ya
tukio baada ya kuamka asubuhi, walishangaa kuona mdogo wake amechelewa
kuamka kwani haikuwa kawaida yake, hivyo walikwenda kugonga mlango na
kukuta ukiwa wazi, walipoiniga ndani wakabaini ameuawa.
Lugata alisema walipiga yowe na majirani wakakusanyika, hatimaye kutoa taarifa kwa uongozi wa Serikali.
Alisema mdogo wake alikuwa amekatwa mguu wa
kushoto kuanzia kwenye goti, amekatwa vidole vitatu vya mkono wa kushoto
na kunyofolewa kucha la dole gumba.
“Dada yangu amekufa kifo kibaya, bora wangemkata
wakamuachia uhai kwani amefariki akiwa tayari ana mimba ya mienzi
mitatu, waliofanya hivyo hawana utu kabisa,” alisema Lugata.
Uongozi kijiji wanena
Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Gasuma, Joshua Mussa
alisema kwa zaidi ya miaka mitatu mwanamke huyo alikuwa akiishi peke
yake na kwamba, aliwahi kuolewa na mwanaume ambaye ni vigumu kumtambu
kwani alikuwa akionekana mara chache.
Mussa alisema mwanamke huyo alikuwa akiishi vizuri na familia, hawakuwahi kusikia migogoro na mumewe waliachana kwa amani.
Aliwataka walemavu hao wanaoishi peke yao, wapewe ulinzi na ndugu zao lakini Serikali inatakiwa kuwaandalia mazingira mazuri.
Naye Diwani wa Viti Maalumu, Hellen Ndibata
alisema mauaji yalikuwa yametulia, hali iliyosababisha Serikali
kujisahau matokeo yake yameanza upya.
Ndibata alisema Serikali inatakiwa kuweka mikakati mahsusi kwa
kuwaandalia mazingira mazuri walemavu hao, kwa kuwaweka kambini kama
walivyofanya kwa wanafunzi albino.
“Mauaji haya yalionekana kuisha hasa kanda yetu ya
ziwa, mwaka huu yanaonekana kuanza upya, ni kazi sasa ya polisi
kuhakikisha watu wanaojihusisha na biashara ya viungo vya albino
wanakamatwa,” alisema.
Wawili mbaroni kwa mauaji
Polisi inaendelea kuwashikilia watuhumiwa wawili
ambao ni waganga wa jadi na kwamba, msako zaidi unaendelea kwa wengine
waliohusika.
Kamanda wa Poilisi Mkoa wa Simiyu, Charles Mkumbo alisema hadi jana walikuwa akiwashikilia waganga hao wa jadi.
“Mganga mmoja kwa mujibu wa ndugu, awali marehemu
alimtuma mtoto mdogo kwenda kwa mganga huyo kuchukua dawa, kwani
marehemu alikuwa akijisikia homa baada ya kufika mtoto huyo kwa mganga
alimweleza shida aliyokuwa ametumwa,” alisema Mkuombo na kuongeza:
“Mganga akamweleza kuwa sema imeisha, lakini
akamwambia leo usilale nyumbani uende kwa mama mkubwa wako, mtoto huyo
hakujua kinachoendelea mpaka mwanamke huyo alipouawa.
Chanzo:Mwananchi
Chanzo:Mwananchi
0 comments:
Post a Comment