Home » » MKUU WA WILAYA YA MASWA ACHOCHEA MOTO

MKUU WA WILAYA YA MASWA ACHOCHEA MOTO


MKUU WA WILAYA YA MASWA ACHOCHEA MOTO

*Wananchi  wasema naye amegeuka kuwa mlalamikaji

 

Na Samwel Mwanga-Maswa

 

HOTUBA ya Mkuu wa wilaya ya Maswa mkoani Simiyu,Luteni mstaafu Abdalah

Kihato aliyoitoa juzi katika ufunguzi wa kikao cha baraza la madiwani

wa halmashauri ya wilaya hiyo imechochea moto  kwa wananchi wa wilaya

hiyo baada ya kuonyesha kuwalalamikia watendaji wanaodaiwa kuhusika na

vitendo vya kifisadi huku  akidaiwa  kuwakumbatia viongozi

waliokataliwa wilayani humo .

 

Viongozi waliokataliwa katika wilaya hiyo mbele ya Naibu Waziri wa

Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI)Aggrey  Mwanri kutokana

na kushindwa kuendesha halmashauri ya wilaya hiyo ni Mwenyekiti wa

halmashauri,Stephen Dwese na Mkurugenzi ,Hilda Lauwo.

 

Wananchi  na Wanasiasa waliozungumza na  Tanzania daima  jana walisema

 Mkuu wa wilaya ameungana na wananchi wa kawaida wilayani humo na kuwa

mlalamikaji, badala ya kutoa mwongozo wa nini cha kufanya kuondokana

na suala hilo na kueleza jinsi ya kulikabili genge la watu hao

wanaotafuna fedha ndani ya halmashauri ya Maswa.

 

Miongoni mwa waliozungumzia hotuba hiyo ni Mwenyekiti wa  Chadema wa

baraza la vijana (BAVICHA) wilayani humo,Peter Shiwa  alisema kuwa

hotuba ya Kihato ilipaswa kujikita katika kuzungumzia masuala

yanayoikabili wilaya hiyo  kwa upana wake na siyo kuvishambulia vyombo

vya habari vinavyoibua uozo ndani ya wilaya hiyo.

 

Alisema mathalani badala ya kuzungumzia utendaji wa vyombo vya habari

juu ya kuibua matatizo ya wananchi wa wilaya hiyo alipaswa kuwaeleza

wananchi kupitia kikao hicho kuwa serikali ya wilaya imejipangaje

kukabiliana na genge la watu wachache walioteka mamlaka ya wilaya hiyo

na kujichotea mamilioni ya fedha bila kushughulikiwa.

 

"Kwangu mimi issue si jinsi vyombo vyahabari vinavyofanya kazi

wilayani humo  bali kinachoniumiza ni  ufisadi ambao ni  dalili ya

ugonjwa mzito unaolikabili taifa,ugonjwa wa kutowajibika, kikundi cha

watu wachache kujilimbikizia mali, mfumo wa sheria kutofanya kazi,

tatizo la watendaji ndani ya halmashauri kufanya mambo wanavyotaka,

watu wanachukua posho hata hawajazifanyia kazi wananchi wa Maswa

wanataka majibu ya maswali hayo'Alisema kwa uchungu.

 

Walisema badala ya kuzungumzia  watu tena kwa mafumbo kwa sababu

vyombo vya habari vimeshaandika juu ya watendaji mizigo ndani ya

halmashauri ya wilaya ya Maswa basi DC alipaswa kuzungumzia bigger

picture (mtazamo mpana) si smaller picture, juu ya matatizo ya wilaya

yetu  angetuhakikishia namna gani serikali yake ya wilaya  imejipanga

katika mapambano dhidi ya ufisadi na siyo kupiga maneno maneno.

 

Walisema  kuwa DC Kihato  hawezi kuepuka mzigo wa tuhuma dhidi ya

viongozi wabovu wilayani humo kwani amekuwa mstari wa mbele kuwatetea

kwa maslahi binafsi  pia anapaswa kuwaeleza Wana Maswa  jinsi

alivyoshindwa kuongoza wilaya hiyo na kubaki kulalamika.

 

"DC hapaswi kulalamika kama anavyolalamika mwananchi wa kawaida katika

hotuba ya juzi amekiri kuwa wapo watu waliokwapua shilingi milioni 20

kama ana ushahidi wa kutosha angeagiza vyombo vya sheria kuchunguza

suala hilo na wahusika wafikishwe mahakamani na siyo kulalamika tu

tena kwa mafumbo huko ni kuonyesha udhaifu katika uongozi wake

"alisema Joseph  John.

 

Walisema kuwa wanasikitishwa na kitendo cha Mwenyekiti wa halmashauri

hiyo,Stephen Dwese kukubali kikao hicho kinachotumia fedha za walipa

kodi wa nchi  hii kugeuzwa kama kijiwe cha mipasho kwani sehemu kubwa

ya hotuba hiyo ilijaa kejeri,matusi na mafumbo hali ambayo

imelishushia heshima baraza hilo.

 

'baraza la madiwani la Maswa  kwa sasa limekosa heshima maana

linageuzwa kuwa kijiwe cha mipasho kutokana na kuruhusiwa kuwepo kwa

vitendo vya kejeri,matusi na mafumbo

 vilivyofanywa wazi na Mkuu wa wilaya huo ni udhaifu wa mwenyekiti wa

halmashauri Mh Dwese kwani hicho si kikao cha DC kwa nini aendelee

kuporomosha matusi naye yupo hapo mezani anachekacheka tu hilo baraza

lina heshima yake ndilo linaloamua mambo ya wananchi wa wilaya

kisigeuzwe kama  kijiwe cha mitaani "alisema kwa hasira Sulu Machibya.

 

Hata hivyo wananchi hao walivitaka vyombo vya habari kutokurudi nyuma

katika utendaji wa kazi zao huku wakiwabeza watu wanaotumia muda wao

kuwatisha waandishi wa habari wanaoibua tuhuma dhidi yao huku

wakisisitiza kuwa vyombo vya habari ndiyo sauti ya wananchi..

 

"vyombo vya habari chapeni kazi kwa maana siye tunaamini habari

mnazoandika au kuzitangaza zina ukweli na usahihi hivyo msiwasikilize

watu wachache wanaowatisha tisha hizo ni changamoto za kazi kumbukeni

utelezi wa mlenda haumwangushi mtu mzima kwani malalamiko

mnayoyaandika au kuyatangaza yanatoka kwetu sisi wananchi ambao

tunanyanyasika au tunaona yana kwenda ndivyo sivyo na mmekuwa msaada

mkubwa sana kwa wananchi"alisema  Eva  Charles.




Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa