Home » » MKOA WA SIMIYU UNATISHA KWA MAAMBUKIZI MAPYA YA VVU

MKOA WA SIMIYU UNATISHA KWA MAAMBUKIZI MAPYA YA VVU


MKOA WA SIMIYU UNATISHA KWA MAAMBUKIZI MAPYA YA VVU

 

Na Samwel Mwanga-Simiyu.

 

MKOA  Wa Simiyu ni miongoni mwa mikoa sita nchini  ambayo inakabiliwa

na maambukizi mapya ya Virusi vya Ukimwi kutoka kwa mama Mjamzito

kwenda kwa mtoto.

 

Hayo yamelezwa jana na Dr Hamis Kulemba ambaye ni Mratibu wa kuzuia

magonjwa ya ngono na Ukimwi mkoa wa Simiyu wakati wa sherehe za

uzinduzi wa  mpango wa kutokomeza maambukizi mapya ya VVU kwa mtoto

kutoka kwa mama mkoani humu katika viwanja wa Sabasaba mjini Bariadi.

 

Dr  Kulemba alisema mpango huo ni mwitikio wa mpango wa kitaifa  wa

utokomeza VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto kutoka asilimia 15 ya

mwaka 2012 hadi kufikia chini ya asilimia nne ifikapo 2015.

 

Alisema mpango huo unalenga kupunguza maambukizi mapya ya VVU kwa

asiliami 50 miongoni mwa wanawake wenye umri wa kuzaa  kati ya miaka

15 hadi 49  na kuongeza na kuboresha upatikanaji wa huduma za uzazi wa

mpango miongoni mwa akina mama wenye maambukizi ya VVU.

 

"Aidha mpango huu utaongeza upatikanaji wa tiba ya ARV kwa akina mama

wajawazito na wanaonyonyesha na kwa watoto walioambukizwa VVU,"

alisema.

 

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa mkoa wa Simiyu,Dr Matoke Muyenjwa  alisema

kwa kupitia mpango huo akina mama wajawazito na watoto wote

walioambukizwa VVU wataanzishiwa dawa za ARV ambazo wataendelea

kuzitumia kwa maisha yao yote.

 

Alisema mpango wa kutoa dawa za kuzuia maambukizi ya VVU uanze,

maambukizi ya VVU toka kwa mama mjamzito kwenda kwa mtoto yanapungua

mwaka hadi mwaka.

 

'huduma ya kuzuia maambukizi toka kwa Mama kwenda kwa mtoto iliendelea

katika wilaya zote mkoani hapa kati ya Januari, 2013 hadi Septemba,

2013 akina mama wajawazito 36,966 walipimwa VVU ambapo kati yao

wajawazito 701 walionekana na VVU sawa na asilimia 2 watoto

waliozaliwa na mama wenye maambukizi ya VVU walikuwa 895 na kati ya

hao watoto 66 sawa na asilimia 7.3 waligundulika kuwa na maambukizi ya

VVU'alisema. .

 

Aliongeza kueleza kuwa wanawake wajawazito wakijifungulia kwenye vituo

vya kutolea huduma serikali itawahakikishia usalama na watapewa elimu

ya namna ya kuzuia maambukizi kwa mtoto na sasa wana vituo 34 kati ya

mahitaji ya vituo 135.

 

Akizindua mpango huo  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Paschal Mabiti katika

hotuba yake iliyosomwa na Mkuu wa wilaya ya Itilima,Bi Geogea Bundala

aliwataka wanaume kutowapuuza wenzi wao wanapokuwa katika kipindi cha

ujauzito na kuambatana nao kliniki ili kupata ushauri wa pamoja kwa

ajili ya kulinda afya zao na afya ya mtoto anayetarajiwa kuzaliwa.

 

Alisema utafiti unaonesha idadi kubwa ya waume wanapuuza kuambatana na

wenzi wao wakati wa mahudhurio ya kliniki sababu kubwa ikiwa ni woga

wa kujua hali ya afya zao na aibu.

 

"Suala la wenzi kuambatana kliniki si jambo la ajabu wala la aibu kwa

kuwa linaongeza uelewa na linasaidia kuijenga familia na jamii katika

suala zima la afya," alisema.

 

Mikoa mingine inayotajwa kuwa na maambukizi makubwa ya VVU  ni pamoja

na Tabora,Kagera,Mwanza,Mbeya na Iringa


Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa