Home » » Wakulima wa pamba waigeuzia kibao serikali

Wakulima wa pamba waigeuzia kibao serikali

Baadhi ya wakulima wa zao la pamba mkoani Simiyu wameanza kukusanya saini zao kwa lengo la kuwasilisha rasmi madai yao mbele ya Serikali na Bodi ya Pamba nchini (TCB) ili waweze kulipwa fi dia kutokana na kuuziwa mbegu ambazo zimegoma kuota.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa waandishi wa habari mwishoni mwa wiki iliyopita na Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima wa Pamba nchini (TACOGA), Elias Zizi alisema hivi sasa wanaendelea kukusanya saini hizo katika Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu na baadaye wataendelea katika wilaya nyingine.
Alisema lengo la kukusanywa kwa saini hizo kutoka kwa wakulima mbalimbali ni kutaka kuwasilisha rasmi madai yao serikalini kuitaka
Kampuni ya Quton iliyopewa kazi ya kuwauzia mbegu za pamba katika msimu wa mwaka huu iweze kuwalipa fidia baada ya mbegu walizouziwa kushindwa kuota na kuwasababishia hasara kubwa.
" Kwa kweli wakulima wamechukizwa na kitendo cha kuuziwa mbegu ambazo zimegoma
kuota pamoja na kupigiwa debe na viongozi mbalimbali wa Serikali wakiwemo wakuu wa mikoa na wilaya pamoja na watendaji wetu wa bodi ya pamba,"
"Walishinikiza kupandwa kwa mbegu hizo zisizo na manyoya kwa madai ndizo zenye ubora na
uhakika wa kuota kwa asilimia 90 ikilinganishwa na zile zenye manyoya ambazo kwa kipindi kirefu ndizo tumekuwa tukipanda na kuota pasipo matatizo, lakini hali imekuwa tofauti, sasa lazima tulipwe fidia," alisema Zizi.
Mwenyekiti huyo alisema wakulima wa zao la pamba wamechoka kila mwaka kuyumbishwa na watendaji wa Serikali ambapo chombo
kilichokabidhiwa dhamana ya kuwasaidia (Bodi ya Pamba) kimeshindwa kutimiza wajibu wake na badala yake hivi sasa kinawasaidia zaidi wanunuzi wa zao hilo.
Alisema baada ya kukamilika kwa kazi ya kukusanya saini hatua itakayofuata itakuwa ni kuwasiliana na wanasheria ili kuwezesha kuyaweka madai yao kisheria zaidi ili wale wote walionunua mbegu zinazosambazwa na Quton na zikagoma kuota waweze kulipwa fidia.
Serikali miaka mitatu nyuma tuliiona jinsi ilivyohangaika kuwalipa fidia wenzetu wenye
kampuni zinazonunua pamba baada ya uchumi wa dunia kuyumba,wengi walilipwa fi dia ya mamilioni ya shilingi, itakuwa ni ajabu kwa Serikali ikatae kuielekeza kampuni ya Quton ili iweze kutulipa fidia, alisema Zizi.
Al i s ema , awa l i wa k a t i viongozi wa Serikali na bodi ya pamba wakihimiza matumizi ya mbegu hizo za Quton wakulima walihoji utofauti na ubora wake unasababishwa na kitu gani kwa
vile mbegu hiyo ni ile ile ya UK.91 iliyozoeleka kwa kipindi kirefu na kwamba iweje itolewe tu manyoya ndiyo iwe bora.
Hivi karibuni kumekuwepo na malalamiko ya wakulima wengi wa zao la pamba katika Mikoa
ya Simiyu, Shinyanga, Geita nabaadhi ya wilaya za Mkoa wa Tabora kulalamikia kitendo cha
kugoma kuota kwa mbegu za pamba zilizosambazwa na Kampuni ya Quton yenye makao yake wilayani Bariadi Mkoa wa Simiy

Chanzo;Majira

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa