SIKU chache baada ya Chama cha Wakulima wa Pamba (TACOGA) kuanza
kukusanya saini za wakulima wa zao hilo wilayani Bariadi, Simiyu kwa
lengo la kuwasilisha rasmi madai yao kwa serikali na Bodi ya Pamba ili
kulipwa fidia kutokana na kuuziwa mbegu za pamba zilizogoma kuota,
kimeungwa mkono na wakulima wa pamba wilayani Maswa.
Wakizungumza na waandishi wa habari waliotembelea baadhi ya vijiji kujionea hali halisi ya mbegu za pamba zisizo na manyoya
zinazozalishwa na Kampuni ya Quton Tanzania Ltd ambazo hazijaota shambani, walisema ni vizuri serikali na Bodi ya Pamba ikawalipa fidia kwa kuwa walikuwa wakiipigia debe kuwa ni nzuri.
zinazozalishwa na Kampuni ya Quton Tanzania Ltd ambazo hazijaota shambani, walisema ni vizuri serikali na Bodi ya Pamba ikawalipa fidia kwa kuwa walikuwa wakiipigia debe kuwa ni nzuri.
“Ni vizuri TACOGA wakafika wilayani Maswa kukusanya na saini zetu ili
tulipwe fidia na serikali pamoja na Bodi ya Pamba kwani hawa ndio
walikuwa mstari wa mbele kututaka tununue mbegu hiyo,” alisema Mwagisu
Mboje, mkazi wa Kijiji cha Zebeya.
Walisema zao la pamba limekuwa halina tija kwa mkulima, kwani hawana
maamuzi kila jambo wamekuwa wakipangiwa kuanzia kulima hadi kwenye soko,
jambo linalowakatisha tamaa kuendelea kulilima. Pia waliitaka serikali
kuivunja Bodi ya Pamba, kwani haina manufaa kwa mkulima.
“Kuna haja gani ya kuwepo kwa Bodi ya Pamba ambayo imekaa kumnyonya
mkulima tu na serikali haiivunji, sie tunabaki masikini lakini wao
wananeemeka?” alihoji Nyanjige Nkongolo, mkazi wa Kijiji cha Mwabayanda.
Kumekuwepo na malalamiko ya wakulima wengi wa zao la pamba katika
mikoa ya Simiyu, Shinyanga, Geita na baadhi ya wilaya za Mkoa wa Tabora
kulalamikia mbegu hizo zilizosambazwa na Kampuni ya Quton kugoma kuota.
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment