Home » » UKOSEFU WA MADARASA NA MADAWATI WATAJWA KUCHANGIA MATOKEO MABOVU

UKOSEFU WA MADARASA NA MADAWATI WATAJWA KUCHANGIA MATOKEO MABOVU

Wadau wa elimu mkoani simiyu wamesema kuwa  kufanya vibaya kwa shule nyingi za msingi na sekondari kunachangiwa na uhaba wa vyumba vya madarasa na madawati.

Hali hiyo imeelezwa na wadau wa elimu mkoani hapa wakati walipokutana katika kikao cha pamoja kujadili hali ya elimu mkoani hapa mjini bariadi.

Wamesema kuwa hali hiyo imekuwa ikichangia kwa kiwango kikubwa shule nyingi kufanya vibaya katika ufaulu wa mitihani yake.

Wadau hao wamesikitishwa na kitendo cha shulenyingi kutokuwa na madawati hali ambayo inawalazimu wanafunzi kuandika kwa ktumia mapaja na wengine kushikilia madaftari mikononi.

Naye  kati bu tawala mkoani hapa bi,mwamvua jilumbi amewataka wadau na watu wengine kujitokeza kubuni njia za kutatua kero zilizopo katika shule za maeneo yao.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa