Home » » MWALIMU SHULE YA MSINGI AUAWA KWA KUPIGWA RISASI

MWALIMU SHULE YA MSINGI AUAWA KWA KUPIGWA RISASI

Mwalimu wa shule ya msingi Mwasengela wilayani Meatu Mkoani Simiyu ameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojilikana.
Tukio hilo limetokea katika kijiji na kata ya Mwaswale tarafa ya Bumera wilayani Itilima mkoani hapa.
Kaimu Kamanda wa Polisi ACP Venance Kimario amemtaja mwalimu huyo kuwa ni Vicent Mganga (67) ambaye ni wa shule ya msingi mwasengela.
Amesema aliuawa kwa kupigwa risasi majira ya saa mbili usiku na mtu au watu wasiojulikana ambao walitoweka mara baada ya kutenda mauji hayo.
kamanda huyo amesema polisi bado inaendelea na uchunguzi juu ya tukio hilo na hakuna mtu anayeshikliwa na polisi..

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa