Home »
» Wakulima wataka Chiza naye ang'oke
Wakulima wataka Chiza naye ang'oke
Sakata
la kuenguliwa mawaziri wanne, limechukua sura mpya baada ya wakulima wa
zao la pamba katika Mikoa ya Simiyu na Shinyanga, kumuomba Rais Jakaya
Kikwete, amwajibishe Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mhandisi
Christopher Chiza.
Wakizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati
tofauti juzi, baadhi ya wakulima hao walipongeza uamuzi wa Rais Kikwete
kuwawajibisha mawaziri hao na kusisitiza kuwa, Mhandisi Chiza naye
anapaswa kuwajibishwa kutokana na kitendo chake cha kuruhusu matumizi ya
mbegu za pamba zilizogoma kuota.
Walisema kitendo cha Mhandisi
Chiza, Wakuu wa mikoa na Wilaya katika mikoa inayolima zao hilo kupigia
debe mbegu za pamba zilizosambazwa na Kampuni ya Quton ambazo
zimeondolewa manyoya wakidai ndizo zenye ubora na baadaye kugoma kuota,
hakistahili kufumbiwa macho.
Mmoja wa wakulima hao, Bw. Christopher
Nhale ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mwabusalu, Wilaya ya Meatu, mkoani
Simiyu, alisema ni muhimu Rais Kikwete akamchukulia hatua Mhandisi
Chiza kwa kuzembea na kusababisha wakulima wengi kupata hasara akidai
mbegu hizo zina ubora mkubwa.
"Binafsi nimepata hasara kubwa,
nilipanda mbegu hizi katika shamba langu lenye ukubwa wa ekari 12,
hakuna hata mbegu moja iliyoota na wakati napanda nilizingatia masharti
yote ambayo niliambiwa, sijui kama Serikali itakuwa tayari kunifidia.
"Viongozi
wetu akiwemo Mhandisi Chiza alizipigia debe mbegu hizi na kuna zingine
zina ubora lakini matokeo yake yamekuwa tofauti...
Waziri
alikurupuka kubariki matumizi ya mbegu hizi ikionesha hakufanya utafiti
wa kina kama kweli zina ubora badala yake aliungana na wenzake
kuzipongeza," alisema.
Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Mwanhuzi,
wilayani Meatu, Elia Shukia alisema hata kama Mhandisi Chiza
atawajibishwa, bado Serikali inapaswa kuwalipa fidia wakulima wote
waliopanda mbegu hizo na kugoma kuota hivyo wamelazimika kupanda mbegu
nyingine upya zilizodaiwa hazina ubora.
N a y e Mw e n y e k i t i w
a Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, mkoani humo, Justin Sheka alisema
umefika wakati wa Serikali kuwathamini wakulima wa zao hilo badala ya
kuwaacha kama watoto yatima wasio na walezi kutokana na usumbufu
wanaoupata katika ulimaji wa pamba.
"Ni vizuri Serikali ikachukua
uamuzi mgumu wa kuwasaidia wakulima wa pamba tofauti na ilivyo sasa,
hawana mtu wa kuwasaidia na pale wanapopata matatizo hawalipwi fidia,
wanunuzi wa pamba uchumi unapoyumba Serikali huwafidia hasara
walizopata," alisema.
Katibu wa Umoja wa Wazee (UWAKA) wilayani
Kahama, Bw. Paulo Ntelya, alisema mbali ya kuwajibishwa mawaziri hao,
Rais Kikwete anapaswa kuwachukulia hatua za kinidhamu watendaji wote
ndani ya Serikali ambao wamehusika kwa njia moja au nyingine kupigia
debe mbegu za Quton na kusababisha wakulima wa pamba wapate hasara.
"Watendaji
wetu ndani ya Serikali, wakuu wa Mikoa, Wilaya na Bodi ya Pamba
walioshinikiza matumizi ya mbegu hizi bila kutoa nafasi ya majaribio,
wanastahili kuchukuliwa hatua za kinidhamu," alisema Bw. Ntelya.
Hivi
karibuni, wakulima wa zao hilo Wilaya za Kahama, Kishapu na Shinyanga,
mkoani Simiyu na baadhi ya maeneo ya Wilaya ya Nzega, mkoani Tabora,
walilalamikia mbegu za Quton kugoma kuota na kusababisha wapate hasara.
Awali,
wakuu wa Wilaya ya Kahama, Nzega mkoani Tabora, Bukombe na Geita mkoani
Geita pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, walihamasisha matumizi ya mbegu
hizo na kuwapiga marufuku wakulima wasipande mbegu zenye manyoya hadi
Rais Kikwete alipoingilia kati sakata hilo
Chanzo;Majira
0 comments:
Post a Comment