
Katika uzinduzi huo uliofanyika juzi jioni
kwenye Uwanja wa Mashujaa wa Bariadi Mjini na kuahirishwa baada ya mvua
kunyesha, Rais alieleza kuwa lengo la Serikali katika uanzishaji mikoa
hiyo na wilaya zake ni kusogeza huduma karibu na wananchi.
Hata hivyo, sherehe hizo ziliendelea jana
asubuhi ambapo Rais Kikwete alisimikwa kuwa Mtemi wa Kisukuma, shughuli
zilizoambatana na maombi ya kuomba baraka ya mvua, hekima, utajiri na
neema kwa ushirikiano wa wazee wa jadi ambao ni watemi wa Kabila la
Kisukuma mkoani humo.
Zoezi la kuuombea baraka Mkoa wa Simiyu pamoja na
kuusimika kijadi, liliendeshwa na Watemi Charles Doto Itale wa Bujashi
akiwa pamoja na Mtemi Andrew Chenge (Itilima) Mbunge wa Bariadi
Mashariki, Wenseslaus Seni (Kanadi), John Ngemela (Magu) waliomvisha
joho na kumkabidhi Utemi Rais Kikwete.
Mkoa wa Simiyu ulianzishwa rasmi mwaka jana na
kuwa mkoa wa nne kati ya mikoa iliyogawanywa katika maeneo mbalimbali
ikiwamo mikoa ya Geita, Njombe pamoja na Katavi hivyo kuifanya Kanda ya
Ziwa kuwa na jumla ya mikoa sita.
Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(Tamisemi), Hawa Ghasia alieleza kuwa Serikali imetenga Sh17 bilioni kwa
ajili ya mkoa huo fedha ambazo amedaiwa ni kwa ajili ya kujenga
miundombinu pamoja na nyumba za watumishi hivyo alitoa wito wa matumizi
yaliyokusudiwa.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment