Home » » Bariadi waanzisha operesheni saka vyoo

Bariadi waanzisha operesheni saka vyoo



SERIKALI wilayani Bariadi, mkoani Simiyu, imetangaza operesheni maalumu kwa ajili ya kusaka familia zisizokuwa na vyoo.
Hatua hiyo imekuja baada ya kugundulika kuwepo kwa familia nyingi hasa za vijijini kutokuwa na huduma hiyo, jambo linalohatarisha kuzuka kwa magonjwa ya mlipuko na uchafuzi wa mazingira.
Operesheni hiyo ilitangazwa juzi na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Erasto Sima, alipozungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani wa halmshauri hiyo.
Alisema operesheni hiyo imelenga kuiwezesha jamii kuchimba vyoo vya kudumu, ili kuepukana na maradhi yanayoweza kuwakumba wananchi, na itaanza muda wowote kuanzia sasa.
“Imegundulika familia nyingi hasa zile za vijijini hapa Bariadi hazina kabisa vyoo. Watu na familia zao wanajisaidia vichakani,” alisema.
Alisema hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya familia zitakazobainika kutokuwa na vyoo, hivyo kuwataka wananchi kuhakikisha wanakuwa na vyoo majumbani mwao.
Pia aliwataka madiwani kuwataarifu wananchi wao kabla ya kuanza kwa msako huo, utakaokwenda kaya kwa kaya, kitongoji kwa kitongoji na kijiji kwa kijiji.

Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa