na Samwel Mwanga, Maswa
WANANCHI
wa Wilaya ya Maswa Mkoa wa Simiyu, wanasubiri kwa hamu vuguvugu la mabadiliko
linalofanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), maarufu kwa jina
la M4C, ili kurudisha kadi za Chama Cha Mapinduzi(CCM) na kukizika chama hicho
wilayani humo.
Wakizungumza
na Tanzania Daima mjini Maswa jana, wakazi hao walisema wamechoshwa na tabia ya
viongozi wa CCM wilayani humo kutotaka mabadiliko huku hawakubaliki katika
jamii hali ambayo imewafanya wananchi kupoteza imani na chama hicho.
“Sasa
binadamu amefikia kikomo cha uvumulivu, viongozi ndani ya CCM wilayani Maswa
hawataki mabadiliko kazi yao ni kung’ang’ania madaraka hebu angalia viongozi
waliokisambaratisha chama ndiyo hao hao wamerudi kushika nyadhifa kwa kutumia
nguvu ya fedha na hawakubaliki ndani ya jamiii,”alisema Masele Mhoja.
Wananchi
hao kutoka katika kata mbalimbali za wilaya hiyo walisema uchaguzi uliomalizika
ndani ya chama hicho ndiyo umechimba shimo la kukizika kutokana na viongozi
waliochaguliwa kuwa vinara wa chuki na fitina.
“Huu
uchaguzi tuliomaliza ndani ya chama ndilo shimo la kukizika chama chetu, kwani
hao viongozi wa ngazi za juu nani asiyewafahamu ndiyo mabingwa wa chuki na
fitina hawataki chama kiwe na mabadiliko ya wasomi ukiwa msomi katika CCM Maswa
wewe ni adui. Kweli tutafika?”alihoji Kada mmoja wa chama hicho, Jishuli
Jidayi.
Wamesema
wamechoshwa na tabia ya viongozi hao ambao katika uchaguzi uliopita
walisababisha majimbo yote ya Maswa Mashariki na Maswa Magharibi kuchukuliwa na
CHADEMA huku wakipoteza Kata tano zilizokuwa chini yao ambao wamegeuzwa kama
kipaza sauti cha mafisadi.
Katibu
wa CHADEMA Wilaya ya Maswa, Luhende Mipawa, alisema lengo ni kuifanya CCM kuwa
chama cha upinzani na kwa kuanzia watahakikisha mamlaka ya mji mdogo wa Maswa
inaongozwa na chama hicho.
Chanzo: Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment