Home » » SERIKALI YATOA MIL.6 KUFIDIA NG’OMBE 22 WALIOPIGWA RISASI SIMIYU

SERIKALI YATOA MIL.6 KUFIDIA NG’OMBE 22 WALIOPIGWA RISASI SIMIYU

Mwandishi wetu, Meatu
SERIKALI imetoa kiasi cha shilingi milioni sita kwa ajili ya fidia ya ng’ombe 22 wanaodaiwa kuuwa kwa kupigwa risasi na askari wa wanyamapori katika pori la akiba la Maswa mkoani Simiyu.

Naibu waziri wa  maliasili na utalii Mhe Lazaro  Nyalandu amesema lengo ni  kurejesha  mahusiano mazuri baina ya askari wa wanyamapori na wananchi wanaozunguka hifadhi hiyo kutokana na uhasama ulioanza kujitokeza baada kuuawa kwa mifugo hiyo.

Akizungumza na baadhi ya wananchi wanaozunguka pori hilo jana,  Mhe Nyalandu amesema wakati taarifa ya tume iliyoundwa kuchunguza mgogoro huo  ikiendelea kusubiriwa, serikali  imeamua  kutoa  fidia  kwa ng’ombe  22 wanaodaiwa kuuwa  kwa kupigwa risasi.

Hata hivyo amewataka wananchi kuzingatia sheria kwa kutoingiza mifugo kwenye pori hilo la akiba
Tangu kuzuka kwa mgogoro huo mwaka 2005, watu sita wakiwemo askari wa wanyamapori wameuawa huku wafugaji kukitozwa faini ya shilingi 72 kwa kuchungia  kwenye pori hilo mwaka  uliopita.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa