Home » » Umeme vijijini utawatoa watanzania katika umasikini

Umeme vijijini utawatoa watanzania katika umasikini

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na: Lilian Lundo – MAELEZO


Injini ya kuinua uchumi wa Tanzania kutoka uchumi wa chini kwenda uchumi wa kati imetajwa kuwa ni uwepo wa umeme wa uhakika unaoendana na mahitaji.

Hayo yamesemwa leo, mjini Dodoma na Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Prof. Sospeter Muhongo alipokuwa akijibu hoja mbalimabli za Wabunge zinazohusu upataikanaji wa nishati ya umeme.

“Bajeti ya mwaka 2016/17 itahakikisha umeme unapatikana vijijini ambapo Wizara ya Nishati na Madini katika bajeti hii imeongezewa asilimia 50 zaidi ya bajeti inayoisha ya mwaka 2015/2016, ili kuhakikisha umeme unapatikana Vijijini,” alisema Mhe. Muhongo.

Mhe. Muhongo aliendelea  kusema kuwa, bajeti hiyo inahakikishha vyanzo vyote vya umeme kama vile gesi asilia, upepo, mawimbi, makaa ya mawe, jotoardhi na jua vinazalisha umeme Nchi nzima.

Aidha, Waziri huyo amesema kuwa bajeti hiyo itapelekea kuboreshwa kwa upatikanaji wa umeme kwa kupitia sheria na taratibu zinazoipa mamlaka TANESCO peke yake kutoa huduma ya umeme kwa kuleta ushindani katika kutoa na kusambaza umeme Nchini.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma  na Utawala Bora, Mhe. Angellah Kairuki akijibu hoja kuhusu swala la kuwepo kwa watumishi hewa na hatua zinazochukuliwa kukomesha tatizo hilo, amesema kuwa Serikali iko tayari kufukuza Maafisa Utumishi wote ambao wamesababisha kuwepo kwa watumishi hewa ili kubaki na Maafisa Utumishi ambao ni wazalendo, waadilifu na wachapakazi.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa