Home » » Simiyu wakamilisha madawati 75%

Simiyu wakamilisha madawati 75%

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

WILAYA ya Maswa, mkoani Simiyu imetekeleza agizo la Rais John Magufuli la utengenezaji wa madawati kwa asilimia 75, asilimia 25 iliyobaki wameeleza kuikamilisha kabla ya Juni 30 mwaka huu.
Hayo yalisemwa jana mjini hapa na Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Rosemary Kirigini wakati akisoma taarifa ya wilaya ya hali ya madawati katika shule za msingi na sekondari kwa Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Antony Mtaka.
Alisema wilaya hiyo inahitaji madawati 26,261 na hadi sasa madawati yaliyopo ni 19,655, hivyo kuna upungufu wa madawati 6,606 na kwa shule za sekondari mahitaji ya meza na viti yalikuwa ni 9,359 na yaliopo ni 10,810 na hivyo kuwa na ziada.
Kirigini alisema pamoja na mafanikio hayo wamekuwa wakikumbana na changamoto mbalimbali zikiwemo za kukatikakatika kwa umeme, kasi ndogo ya upatikanaji wa mbao, uhaba wa fedha na ushiriki mdogo wa wadau mbalimbali katika kuchangia utengenezaji wa madawati.
Aidha alisema katika kutekeleza agizo hilo wilaya hiyo imejiwekea mikakati ili kuondoa tatizo la upungufu wa madawati ambayo ni pamoja na kukarabati madawati yote mabovu, kununua mbao 29,748 na kuzipeleka Chuo cha Ufundi (Veta) cha Binza kilichoko wilayani humo.
Alisema Sh 475,968,000 kutoka vyanzo vya mapato ya ndani ya halmashauri zitatumika kutengeneza madawati hayo.
Naye Mkuu wa Mkoa pamoja na kuwapongeza kwa ubunifu wa kukitumia Chuo cha Ufundi cha Binza kutengeneza madawati, alisema huenda wilaya hiyo ikawa ni miongoni mwa wilaya zitakazoongoza kwa utekelezaji wa agizo hilo la rais.
Chanzo Gazeti La Habari Leo
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa