Home » » KAMPENI ZA CCM ZAPAMBA MOTO,MWIGULU,LOVENESS MAMUYA WASHIRIKI UFUNGUZI WA KAMPENI KISESA-MEATU

KAMPENI ZA CCM ZAPAMBA MOTO,MWIGULU,LOVENESS MAMUYA WASHIRIKI UFUNGUZI WA KAMPENI KISESA-MEATU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mwigulu Nchemba na Mgombea Ubunge Jimbo la Kisesa-Meatu Ndg.Mpina wakiwasili Uwanja wa Mkutano hii leo wakati wa Ufunguzi wa kampeni katika Jimbo hilo.Mapokezi ya Mgombea Ubunge Jimbo la kisesa wakati wa Mkutano wa kufungua kampeni za Ubunge na Udiwani hii leo.Mwigulu NChemba akisalimiana na Wananchi wa Kisesa hii leo alipokwenda kufanya ufunguzi wa kampeni katika Jimbo hilo.Makada wa chama cha Mapinduzi wakifuatilia Mkutano wa Kufungua Kampeni Jimbo la Kisesa.Kada Mtiifu wa Chama cha Mapinduzi Loveness Mamuya "Iron Lady" anayeishi Nchini Marekani ameshiriki tukio la Ufunguzi wa Kampeni wa Jimbo la Kisesa na Zaidi amekuwa akishiriki kampeni zinazoendelea za Uchaguzi Mkuu wa nafasi ya Madiwani.Ubunge na Urais Nchini.Loveness Mamuya amewaomba Watanzania na Wananchi wa Kisesa kuhakikisha wanafanya Uchaguzi wa Amani,Watu wajitokeze kupiga kura na Waichague CCM katika nafasi zote tatu kwakua ndio chama chenye Dira na Ilani bora ya kuinua Maendeleo ya Wananchi.,Mbali na hilo Mamuya alisisitiza kuwa atatumia Ukada wake wa Chama cha Mapinduzi kuendelea kuwashawishi Watanzania kuhakikisha Magufuli anashinda nafasi ya Urais kwakua rekodi ya Uchapakazi wake inaleta matumaini kuwa Tanzania inakwenda kusonga mbele.Mwigulu Nchemba akibadilishana mawazo na Mgombea Ubunge Jimbo la Kisesa Ndg.Mpina.Mwigulu Nchemba ambaye ameshiriki zoezi la Ufunguzi wa kampeni Jimbo la Kisesa,Amesisitiza Watanzania kuachana  na Walaghai wa kisiasa kuhusu Mabadiliko,Amesema amabadiliko ya kimaendeleo ndio ya kuzingatia na sio Vyama vya Siasa.Tanzania ya Mwaka 1961 na ya leo 2015 katika elimu,Afya,Miundombinu n.k imebadilika sana,Hivyo CCM bado inanguvu ya kuhakikisha kasi ya Kuleta maendeleo inaongezeka .Pia amesisitiza Wananchi kujitokeza kupiga Kura kumchagua Mgombea Urais wa CCM Ndg.J.Pombe Magufuli na Wabunge/Madiwani wote wa CCM.Sehemu ya mamia ya Wananchi wakishangilia hotuba ya Comrade Mwigulu Nchemba.Mh.Mpina akiwa na Wazazi wake wote wawili wakati akiomba ridhaa ya kuongoza tena jimbo la Kisesa,Kuba ameahidi kuboresha Elimu kwa kuhakikisha anasambaza mfumo wa kutumia Computer kwenye shule zote kwasababu alishawanunulia Sola za Umeme kwa kila Shule,Pia uboreshaji wa maji kwa kuvuta kutoka Shinyanga kwenye mradi mkubwa unaotokea Ziwa Victoria,Zaidi amesisitiza kuhakikisha Barabara za jimbo la Kisesa zinafikia kiwango cha Rami.Mh.Mpina akiwa na Kada wa Chama cha Mapinduzi kutoka DMV Marekani Bi.Loveness Mamuya.Chama cha Mapinduzi kwa Tanzania ndio chama pekee chenye Mtandao Mkubwa wa ndani ya Nchi na hata Nje ya Nchi,sababu inayopelekea CCM kuwa na Wafuasi wengi kuliko chama chochote kile hapa Tanzania.
Picha na Sanga Festo Jr

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa