Home » » WATAKIWA KUWA WABUNIFU KUJILETEA MAENDELEO

WATAKIWA KUWA WABUNIFU KUJILETEA MAENDELEO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

VIJANA mkoani Simiyu wametakiwa kuacha kujiingiza katika makundi hatarishi, na badala yake wawe wabunifu kwa lengo la kujiletea maendeleo.
Hayo yalisemwa hivi karibuni na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) Mkoa wa Simiyu, Njalu Silanga, katika sherehe ya uwekaji jiwe la msingi katika ofisi ya wajasiriamali ya Nyasubi SACCOS mjini Bariadi.
Alisema vijana wengi wamekuwa na dhana ya kuilalamikia Serikali kuwa haijawaletea maendeleo, hali inayosababisha wengi wao kukaa vijiweni ikiwa pamoja na kuingia katika vikundi vya kuhatarisha maisha yao.
Njalu alisema kuwa maendeleo kwa kila Mtanzania yanakuja kwa kila mmoja kuwa mbunifu pamoja na kujishughulisha katika kazi mbalimbali sambamba na kujiunga katika vikundi vya ujasiriamali.
Mwenyekiti huyo ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa uwekaji jiwe la msingi katika ofisi hiyo alisema ni vyema vijana wakawa wabunifu pamoja na kujiunga katika vikundi mbalimbali vya wajasiriamali ili kujiletea maendeleo. Awali akisoma risala kwa mgeni rasmi Katibu wa wajasiriamali wa Nyasubi SACCOS, David Wambura, alisema kuwa tangu kuanzishwa kwa asasi hiyo jumla ya wanachama 214 wamejiunga huku wanawake wakiwa 132 na wanaume wakiwa 82.
Alisema asasi hiyo imelenga kuwaletea maendeleo wanachama wote kwa kujikopesha ndani ya asasi yenyewe ili kuhakikisha kuwa wanaweza kujiletea maendeleo

Chanzo:Majira

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa