Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
MIRADI 60 ya hifadhi mazingira iliyopo katika vijiji 8 vya Wilaya
ya Itilima, mkoani Simiyu yenye thamani ya sh bilioni moja,
imekataliwa na madiwani wa wilaya hiyo.
Miradi hiyo mikubwa ya hifadhi mazingira bonde la Ziwa Victoria awamu
ya pili (LIVEMP II) imeendelea kukataliwa kwa kile kinachodaiwa
wananchi kunyang’anywa maeneo yao.
Hali hiyo ilijitokeza katika semina iliyoandaliwa na shirika lisilo
la kiserikali la Livemp, wilayani Itilima ambapo baadhi ya viongozi hao
wakiwemo madiwani walisema mradi huo hauna faida kwa wananchi.
Walieleza wananchi wao mbali na kunyang’anywa maeneo yao, elimu ya
umuhimu wa mradi huo haijatolewa kwa kiwango cha kutosha ikiwa pamoja
na fidia kwa walionyang’anywa maeneo yao.
“Mradi huu wa hifadhi mazingira upo kisiasa, na kwamba wananchi wa
maeneo ambayo miradi hiyo inapita hawajapatiwa msaada wowote, hata
kuwapelekea miti ya matunda, ili waache kulima katika kando ya mito na
badala yake wamenyang’anywa maeneo hayo bila ya kupewa fidia,” alisema
Diwani Nestuta Mlyandengu.
Awali akizungumza katika mradi huo kwa niaba ya mkurugenzi wa shirika
hilo, Nesphory Subira, alisema mradi huo utawasaidia wananchi wa
maeneo wanayopitiwa na miradi hiyo kwa kuwa watapatiwa miti ya matunda
kwa ajili ya kupanda kando kando ya mito pamoja na miti mingine kwa
ajili ya kuhifadhi mazingira.
Mkuu wa wilaya hiyo, Geogina Bundala, alishangazwa na hatua ya
madiwani hao kuikataa miradi hiyo ambayo ingewasaidia wananchi katika
kuwaondolea umasikini.
Chanzo:Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment