Home » » BARIADI WAKUBALI TIKA

BARIADI WAKUBALI TIKA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WADAU wa afya katika Halmshauri ya Mji wa Bariadi, mkoani Simiyu, wameridhia kutumika kwa mfumo mpya wa utoaji wa huduma za afya kwa kadi (TIKA).
Wadau hao walifikia uamuzi huo jana kwenye warsha iliyofanyika kwenye ukumbi wa Kanisa Katoliki mjini Bariadi.
Mbali na kuridhia kutumika kwa mfumo huo ambao uko chini ya Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), wadau hao wamedai  ili kupatikana mafanikio ya kutumika kwa mfumo huo ni vema  kuwepo kwa usimamizi mkubwa wa fedha zitakazotokana na huduma hiyo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, walisema uanzishwaji wa Tika utasaidia wananchi kutibiwa kwa uarahisi kuliko ilivyo sasa ambapo huangaika katika kutafuta fedha za matibabu.
“Tunaipongeza serikali kwa kuleta mfuno huu, kwani unalenga kutatua kero waliyonayo ya kila siku katika kupata huduma za afya,” alisema Selina Deusi.
Akitoa maelezo ya juu ya faida ya mfumo huo, Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Elltruder Mbogolo, alisema lengo la kuletwa kwa mfumo huu ni kupunguza kero za upatikanaji wa dawa pamoja na vifaa tiba katika vituo vya afya na hospitali.
Akifungua warsha hiyo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Katibu Tawala wa mkoa huo, Mwanvua Jirumbi, amewataka viongozi wa halmashauri zote kuhakikisha wanasimamia ipasavyo mradi huo, ili uweze kuwanufaisha wananchi.
Chanzo;anzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa