Home » » MABITI ADAIWA KUJIPACHIKA UTEMI

MABITI ADAIWA KUJIPACHIKA UTEMI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
John IlemeUKOO wa Chifu wa Dutwa umemtaka Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Pascal Mabiti, kutengua utemi wa Bahunda aliojipachika bila ridhaa ya ukoo huo.
Akizungumza kwa niaba ya ukoo huo na Tanzania Daima, jijini Dar es Salaam juzi, John Ileme, alisema Mei mwaka jana, Mabiti alijitawaza kuwa Mtemi wa Dutwa kupitia mgongo wa jamii ya Wasukuma wachache wa ukoo wa Bahunda kinyume cha utamaduni wa jamii hiyo.
Alisema wanamtaka afanye hivyo kwa sababu ukoo wa Dutwa haumtambui kuwa ni mwanaukoo, na kwa utaratibu wa mila na desturi hana sifa ya kuwa mtemi wa utemi huo.
Ileme alisema endapo atashindwa kufanya hivyo kwa hiari yake, Chifu wa  Dutwa na ukoo wa Bahunda wa Dutwa hautasita kuchukua hatua za kisheria, ikiwa ni pamoja na kumfikisha mahakamani.
  Chaanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa