
Dk. Kamani juzi alifanyiwa sherehe za kupongezwa zilizoandaliwa na
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Busega kwa kushirikiana na Mkoa wa
Simiyu baada ya kuapishwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa waziri wa wizara
hiyo.
Akiwa katika Kata ya Mkula, Chama cha Wavuvi Mkoa wa Mwanza
walimwelezea waziri changamoto mbalimbali zinazowakabili zikiwemo za
rushwa ndani ya wizara hiyo.
Akieleza changamoto hizo kwa niaba ya wavuvi wenzake wa Mwanza,
Robert Sijaona, alisema wao wana nia ya dhati na serikali, lakini wapo
wanyonyaji wachache wanawaangusha kwa kuwakandamiza.
Alitaja changamoto nyingine kuwa ni uvuvi haramu unaotokana na wavuvi hao kutumia mabomu na nyavu haramu.
Alisema ujambazi unaowaumiza ni ule uliokithiri katika Ziwa Victoria
ikiwa ni pamoja na kuporwa nyavu zao pamoja na boti za uvuvi.
“Sisi wavuvi tukiwezeshwa tunaweza tutapambana saa 24, hivyo
tunaamini kuwa mkombozi wa wavuvi wetu ni wewe Dk. Kamani na tuna imani
utatuinua,” alisema Sijaona.
Alisema changamoto nyingine ni katika rushwa kwa wafanyabiashara wakubwa kutokana na kuwakandamiza wafanyabiashara wadogo.
Pia walimwelezea Dk. Kamani kuwa na tatizo kubwa la upatikanaji wa
soko nje ya nchi huku wakieleza endapo wakipata soko kiurahisi wao ni
matajiri wakubwa.
Naye Brida Mshota kutoka katika Chama cha Wafugaji Tanzania (CCWT)
nao walielezea changamoto yao kuwa ni kukosa elimu na faini kubwa endapo
wakifikishwa mahakamani na kwamba hawana watetezi.
Pia alisema maeneo ya wananchi yamechukuliwa na serikali ikiwa ni
pamoja na maeneo aliyoyataja kuwa ni pori la Maswa, Bunda, Bariadi na
mapori mengine.
Akijibu, Waziri Kamani alisema kuwa atajitahidi kadiri ya uwezo wake kuhakikisha matatizo yanapungua au kwisha kabisa.
Dk. Kamani alisema wakati anaingia wizarani hapo amekuta kuna
changamoto nyingi, ikiwa ni pamoja na wafugaji na wakulima kufikia
wakati hata kuuana.
Alisema ameagiza watendaji wa wizara kuwasiliana na watendaji wa wilaya kufahamu matatizo mbalimbali yanayowapata katika maeneo.
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment