WANANCHI
katika mkoa wa Simiyu, wametakiwa kushirikiana na serikali, ili
kukomesha vitendo vya uhalifu, vikiwemo vya ujangili katika hifadhi za
taifa na mauwaji ya vikongwe na watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino) kwa
imani za ushirikina pamoja na ukeketaji wa watoto wa kike.
Mkuu wa mkoa wa Simiyu Bw. Paschal Mabiti, ametoa rai hiyo juzi katika
eneo la Stop over, karibu na hifadhi ya taifa ya Serengeti, wakati
akihutubia wananchi, baada ya kufunga mashindano ya Serengeti Marathon
mwaka 2013.
Bw. Mabiti aliyekuwa anamwakilisha waziri mkuu Mizengo Pinda, amesema
kuwa kuna ujangili wa kutisha katika hifadhi za taifa, ambapo majangili
yamekuwa yakiua wanyama mbalimbali wakiwemo Faru na Tembo, hali ambayo
inahatarisha kutoweka kwa wanayama hao.
Aidha, amesema kuwa ni jukumu wananchi wote mkoani hapa, kushirikiana na
serikali ili kukomesha ujangili huo, pamoja na vitendo vingine vya
uhalifu, hususan mauwaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Abino) pamoja
na vikongwe kwa imani ya ushirikina.
Amesema kuwa pia ni wajibu wa wananchi wote kupiga vita ukeketaji wa
watoto wa kike kwani hali hiyo inahatarisha maisha yao.
Amesema kuwa iwapo wananchi wote mkoani hapa wakishirikiana na serikali,
katika kuhakikisha wanaimarisha uhifadhi, ikiwa ni pamoja na kuwataja
bayana wanaoendesha vitendo hivyo,, hali hiyo inaweza kudhibitiwa na
hifadhi zetu kuwa endelevu.
Mbali na kuhifadhi hifadhi ya taifa ya Serengeti na maeneo tengefu, pia
aliwataka wananchi kuhifadhi ziwa Victoria, ili liweze kuwa endelevu kwa
kuacha uvuvi haramu ambao unahatarisha viumbe hai vya majini.
Mapema mbunge wa jimbo la Busega, ambaye pia ni mwenyekiti wa chama cha
mapinduzi mkoani Simiyu, Dk. Titus Kamani, aliyeandaa mashindano hayo
kwa ajili ya kutangaza utalii na kuhamasisha uhifadhi endelevu, amesema
kuwa vitendo vya uwindaji haramu vimekuwa vikisababisha kuharibu uchumi
wa nchi.
Dk. Kamani amesema kuwa iwapo hali hiyo haitadhibitiwa ipasvyo, upo
uwezekano mkubwa wanayama kumalizika na hivyo kukosa fursa ya kupata
watali ambao wamekuwa wakiingizia taifa fedha nyingi za kigeni.
Amesema kuwa pia mauwaji ya Albino na vikongwe kwa imani za ushirikina
na ukeketaji wa mtoto wa kike, ni vitendo ambavyo kwa kiasi kikubwa
vinauchafua mkoa huo wa Simiyu, na hivyo kamwe haviwezi kuvumiliwa.
Home »
» Wananchi Simiyu watakiwa kukomesha ujangili, mauaji ya Albino, Vikongwe
0 comments:
Post a Comment