Home » » Bodi ya pamba yatakiwa kupeleka mbegu mbadala

Bodi ya pamba yatakiwa kupeleka mbegu mbadala

Meatu. Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, mkoani Simiyu, wameomba Bodi ya Pamba kuweka utaratibu wa kusambaza mbegu mbadala ya zao la pamba, baada ya zilizosambazwa na Kampuni ya Quton kubainika hazioti katika maeneo ya wilayani hapa.
Wakichangia hoja kuhusu maandalizi ya kilimo msimu wa mwaka huu kwenye kikao cha Baraza la Madiwani juzi, madiwani hao walisema mbegu za Quton zilizopigiwa debe kuwa ni ubora zimegoma kuota katika maeneo mengi.
Kutokana na hali hiyo, walisema kuna kila sababu ya bodi ya pamba hivi sasa itafute mbegu mbadala ili kuwezesha wakulima kuwahi kupanda kabla ya Desemba 20.
Walisema bila kuchukuliwa hatua, vinginevyo hali ya kilimo cha pamba msimu huu itakuwa mbaya.
Walisema mbegu hizo zilizopandwa baada ya kuitikia wito wa viongozi zimekataa kuota katika kata za Mwabusalu, Mwanyahina, Mwabuzo, Imalaseko na Nkoma.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa