Home » » CHADEMA WAMFUKUZA SHIBUDA

CHADEMA WAMFUKUZA SHIBUDA


Katika hali isiyo ya kawaida, Mbunge wa Maswa Magharibi, mkoani Simiyu, Bw. John Shibuda, juzi alijikuta katika wakati mgumu baada ya kupigiwa kura za kumtaka atoke nje ya ukumbi wa mkutano ambao uliandaliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kwa lengo la kuchagua viongozi wa Kanda ya Ziwa Mashariki akidaiwa ni msaliti.
 Hali hiyo ilitokana na hoja iliyotolewa na mjumbe mmoja ndani ya kikao hicho ambacho kilifanyika Mjini Shinyanga kikiongozwa na Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Bw.Freeman Mbowe.
Mjumbe huyo alisimama na kuomba Bw .Shibuda atolewe nje ya kikao akidai haaminiki na mara nyingi amekuwa akitoa siri za chama hicho kwa viongozi wa CCM.
Hatua ya kutimuliwa kwa Shibuda ilikuja muda mfupi baada ya Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA kufungua kikao hicho ambapo mjumbe huyo kutoka Mwibara Bunda mkoani Mara, Ahmed Nkunda alisimama na kutoa hoja yake lakini hata hivyo Shibuda aliamua yeye mwenyewe kutoka ili kuepusha vurugu.
Kitendo cha kutolewa nje Bw. Shibuda,kilisababisha kundi kubwa la wajum be wengine kumfuata wakionesha wazi kutounga mkono hoja ya mjumbe mwenzao na ku onesha mpasuko wa wazi ndani ya chama hicho kikuu cha upinzani nchini.
Hata hivyo, kabla ya Bw. Shibuda hajatoka nje, Bw, Mbowe alimuomba asitoke ndani ya kikao hadi awahoji wajumbe wengine kam a wanaafiki hoja hiyo ili kujua ni wangapi wanaunga mkon o na wangapi wanataka aendelee kuwepo.
Matokeo ya kura hizo yalionesha wajumbe 90 waliunga mkono aondoke ndani ya kikao na 30 wakitaka aendelee kubaki ambapo baadhi y a wajumbe walisema,Bw. Mbowe alishindwa kusimamia mchakato huo kwani se hemu kubwa ya wajumbe waliotaka Bw. Shibuda abaki hawakuhesabiwa.
Mmoja wa wajumbe waliotaka mbunge huyo ab aki(jina tunalo ), alisema uhesabuji kura uliofa nywa na Bw. Mbowe haukuwa sahihi kwani kura hizo ziliegemea upande mmoja ndiyo sa babu ambayo ilichangia wajumbe wengine kuon doka ndani ya ukumbi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Bw.S hibuda alidai kusikitishwa na kitendo cha kutole wa nje ya kikao kwa kupigiwa kura wakati yeye mwenyewe alishaafiki kutoka nje kwa hiari yake ili kuepusha kuvurugika kwa kikao hicho.
“Kilichoniponza hadi nionekane msaliti ndan i ya chama ni kitendo changu cha kuwatetea wakulima wa zao la pamba na wafugaji katika jimbo langu. ..hivi karibuni nilifikisha kilio chao kwa Katibu Mkuu wa CCM Taifa,Abdulrahman Kinana.
“Mimi si msaliti kwa kile nilichokifanya bali natetea hakina masilahi ya wapiga kura wangu, wakulima na wafugaji, pale Meatu nilipanda katika jukwaa la CCM kumweleza Kinana matati zo ya wapiga kura wangu maana yeye ndiye mwenye Serikali iliyoko madarakani kwa sasa,”alisema Bw. Shibuda.
Aliongeza kuwa, hakuna njia ya mkato ya wananchi kutatuliwa kero zao bila ya kupitia chama tawala ambapo wakulima wa pamba na wafugaji, wanahitaji tiba badala ya maneno m atupu ya ukuwadi na uwakala wa kuwa pumbaza kisiasa hivyo utatuzi wa matatizo yao ni Serikali ya CCM iliyoko madarakani.
Bw.Shibuda alisema utetezi wake kwa wapig a kura umemfanya aonekane msaliti,Bw. Mbowe aliwahi kumpongeza Rais Jakaya Kikwete kwa kazi nzuri ya kuwapelekea maendeleo wananchi wa jimbo lake sasa kwa nini asionekane msaliti.
“Kwangu mimi,masilahi ya wafugaji na wakulima wa zao la pamba ndiyo kipaum bele changu cha siasa za uokovu na ukombozi, kama ingebidi kwenda kwa shetani kutafuta tiba ya matatizo yao hakika ningekwenda achilia mbali CCM, kwa sasa chama tawala ndiyo chenye tiba hatuwezi kuwakwepa,” alisema Bw. Shibuda

CHANZO;MAJIRA

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa