WAJASILIAMALI
120 walioko katika wilaya za Busega na Magu, waliokopeshwa kiasi cha sh. 72
milioni kwa masharti nafuu na shirika moja lisilokuwa la kiserikali la Rural
Initiatives and Relief Agency (RIRA) lililofadhiliwa na serikali ya Marekani,
wameshindwa kurejesha fedha hizo na sasa shirika hilo litawafikisha mahakamani.
Mkurugenzi
wa shirika hilo lenye makao yake makuu katika katika kijiji cha Kabita wilayani
Busega, mkoani Simiyu, Bw. Johnson Rollas, amesema kuwa watu hao walikopeshwa
fedha hizo mwaka juzi na walitakiwa kuzirejesha mwezi septemba mwaka jana ili
wananchi wengine waweze kukopeshwa.
Bw.
Rollas amesema kuwa wananchi hao wakiwemo maafisa watendaji wa vijiji na kata,
wenyeviti wa vitongoji na mitaa na wanachama wa vikundi wa wajasiliamali
walikopeshwa pesa hizo kwa ajili ya kufanyia biashara ndogondogo, ikiwa ni
pamoja na kilimo cha bustani, ufugaji wa kuku pamoja na upandaji miti, baada ya
kuweka dhamana ya mali zao zisizohamishika yakiwemo mashamba na nyumba.
Amesema
kuwa wananchi hao walikopa mikopo hiyo kati ya shilingi milioni moja hadi
milioni tatu na kwamba fedha hizo zilitakiwa zirejeshwe kwa riba ya asilimia
tano na kisha kukopeshwa watu wengine na baadaye kurejeshwa kwa wafadhili hao
baada ya awamu hiyo ya kwanza kuwa imemalizika.
Aidha,
mkurugenzi huo amesema kuwa watanzania hao wameliabisha taifa kwa kukopa fedha
za wafadhili na kushindwa kuzirejesha na kwamba sasa shirika lao linaiomba
serikali kuingilia kati, ili wakopaji hao waweze kurejesha fedha hizo ndani ya
siku 14 kabla ya kufikishwa mahakamani.
Amesema
kuwa serikali ya Marekani imeshindwa kutoa fedha nyingine kwa shirika hilo
kutokana na wakopaji hao kutokurejesha fedha hizo za kwanza na hivyo kufanya
shirika lao kutokuaminiwa na wafadhili hao.
Ameongeza
kuwa iwapo wananchi hao wakishindwa kurejesha pesa hizo kwa muda ambao ni
wanyongeza wa siku 14, utakapokuwa umeisha watapeleka suala hilo mahakamani na
kwamba mali zao walizoweka dhamana zinaweza kuuzwa na hivyo hali hiyo inaweza
kuleta mtafaruku mkubwa katika jamii na familia zao kwa ujumla.
0 comments:
Post a Comment