Home » » MVUA YAHARIBU MAKAZI YA WATU 92 KATA YA BADI

MVUA YAHARIBU MAKAZI YA WATU 92 KATA YA BADI

ZAIDI ya watu 92 katika kata ya Badi wilayani Maswa wamekosa mahali pa kuishi kufuatia nyumba zao kuaribiwa na mvua zinazoendelea kunyesha.

Mtendaji wa kata hiyo Gervas Nywage,amesema uharibifu huo umetokea katika vijiji vya Muhida na Jihu kwa nyakati tofauti katani humo.

Amesema katika uharibifu huo zaidi ya nyumba 102 zikiwemo zilizoezekwa kwa nyasi 44 zimearibiwa na mvua iliyoambatana na mafuriko.

Mtendaji huyo amesema katika uharibifu huo yamo mashamba ya mazao na vyakula  ikiwemo miundominu ya barabara.
Naye Diwani wa Kata hiyo Bw Martine Masele ameiomba serikali kupitia ofisi ya waziri mkuu kitengo cha maafa kuwapelekea wahanga hao misaada ikiwemo vyakula.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa