Home » » SAFISHA MJI YAPAMBA MOTO WILAYANI MASWA

SAFISHA MJI YAPAMBA MOTO WILAYANI MASWA

Mwandishi wetu, Maswa-Simiyu Yetu
Mamlaka ya Mji mdogo katika Halimashauri ya Wilaya ya Maswa imeamua kuwaondoa Wafanyabishara kwa nguvu katika maeneo ambayo hayaruhusiwi kufanya Biashara kwa mujibu wa Sheria ndogo ndogo za Mji huo
Kauli hiyo imetolewa na Kaimu Afisa Mtendaji wa Mamlaka ya Mji mdogo Maswa Bibi Veronica Nestory wakati akiongea na Radio Free Africa Mjini Nyalikungu Maswa leo
Bibi Veronica pamoja na mambo mengine amesema Mamlaka yake imeunda timu ya Watalaamu wa Mamlaka wanao simamia zoezi la kuwaondoa Wafanya biashara kwa msaada wa walinzi wa amani (Polisi) kwa ajili ya Wafanyabishara
 Ambao wamendelea kukaidi amri halali iliotolewa na Mamlaka kwa muda mrefu ya kuwataka kuondoka maeneo yasiyo ruhusiwa kuendesha biashara kinyume cha sheria na kwenda kufanyia shughuli zao katika maeneo waliopangiwa na Mamalaka yake
Kaimu Afisa Mtendaji huyo ameyataja maeneo hayo kuwa ni pamoja na kuzunguka eneo la uwanja michezo nguzo nane, Njiapanda na eneo la Binza kwa ajili ya kuoshea magari
Aidha akibainisha zaidi kuwa Wafanya bishara watakoa husika na oparesheni hiyo kuwa ni Mafundi Baiskeli,Wauza mitumba,wauzaji wa vifaa vya ujenzi kama vile mbao,Saruji,Nondo,mabati vitu vingine ni Chokaa weld meshi na Wenye magereji ya Magari na Pikipiki
Amesema zoezi hilo ni endelevu na amewaonya watu wakao puuza agizo hilo Mamalaka ya yake haitasisita kuwafikisha katika vyombo vya Dola ili mkondo wa sheria upite
Blogzamikoa

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa