Home » » MADIWANI WALALAMIKIA ASKARI WA USALAMA BARABARANI BARIADI

MADIWANI WALALAMIKIA ASKARI WA USALAMA BARABARANI BARIADI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

madiwani wa halmashauri ya wilaya ya bariadi mkoani simiyu wamelalamikia kitendo cha askari wa usalama  barabarani kuwakamata watu wanaosafirisha abiria kwa pikipiki (bodaboda) kinyume cha sheria.
 hayo wameeyaeleza leo katika kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa barideko mjini bariadi.

wamelalamikia kitendo cha askari wa usalama barabarani kuwakamata bodaboda kinyume na taratibu za jeshi la polisi.

wameeleza kuwa baadhi ya askari hao wamekuwa wakikaa katika maeneo yasiyo rasmi na kisha kuwasimamisha waendesha bodaboda hali ambayo imekuwa ikisababisha  ajali na majeraha kwa wahusika.
 akijibu malalamiko hayo mkuu wa wilaya hiyo erasto sima ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalam ya wilaya amelaani kitendo hicho na kuahidi kulifuatilia ikiwemo kutoa mafunzo kwa waendesha bodaboda wote.
 amewataka pia askari wa usalama barabarani kuzingatia kanuni,sheria na taratibu za kazi yao

 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa