Home » » MWANRI AMSIMAMISHA KAZI MHANDISI WA H/SHAURI

MWANRI AMSIMAMISHA KAZI MHANDISI WA H/SHAURI

NAIBU Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI), Bw.Aggrey Mwanri , amemsimamisha kazi Kaimu Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima, mkoani Simiyu, Paschal Manyama.
Bw. Mwanri alichukua uamuzi huo baada ya kubaini kuwa, mradi wa barabara inayoingia katika Ofisi za halmshauri hiyo yenye kilomita 1.03, imejengwa chini ya kiwango.
Barabara hiyo imejengwa na Mkandarasi Virgin Company Limited ambayo ujenzi wake uligharimu zaidi ya sh. milioni tisa bila kuweka mitaro na baada ya kuulizwa na Bw. Mwanri, hakuwa na jibu la kuridhisha.
Wakati akiendelea kukagua mradi huo, alibaini kuwepo kasoro nyingi ikiwemo ya mkandarasi huyo kutopewa mkataba na mchoro unaonyesha gharama za mradi (BOQ).
Bw. Mwanri alipata mashaka na utendaji kazi wa mhandisi huyo kutokana na majibu yake kutokuwa ya kitaalamu na kumwagiza Katibu Tawala Mkoa, Mwanvua Jilumbi kumwondoa katika nafasi aliyonayo na kumtafutia kazi nyingine.
"Namsimamisha kazi huyo mhandisi, hafai hata kidogo kuwa katika nafasi hii ndiyo maana nauliza maswali yanamshinda, kama ataendelea kukaa hapa, halmashauri itapata hasara.
"Katibu Tawala Mkoa tafuta mtu mwingine na huyu mhandisi mpangieni kazi nyingine si hii,"
alisema

Chanzo:Majira

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Simiyu Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa